Mpasho Exclusive: Nyota Ndogo Attacked By Her Dancers For Dumping Them Like Rubbish

Piece by: Kwarula Otieno
Entertainment

A renowned dance group from the coast has come out to accuse Mombasa-based top female artist Nyota Ndogo for dropping them. 

All Saints Dance Crew claims that they had an agreement with Nyota Ndogo, that they would appear on her next 2 videos, one of them featuring P-Unit's Frasha.

The also says that they went through a lot practising for the 2 videos but when the time to shoot the video came, Nyota Ndogo went silent on the last minute.

"Tafadhali twaomba muangazie hili jambo . . . Nyota Ndogo atema ma dancer wake Hili ni jambo linakera sana ila ni vyema kujua si vita ama ubaya na mtu anapohishi jambo linalo mkera kulisema. Ndio maana inabidi jambo kama hili liwe wazi kwa mafans na kila mmoja ambaye anafahamu usanii na sanaa. All Saints Dance Crew kikundi tajika Pwani nzima na Taita Taveta haswa, kikundi chenye uwezo mkubwa kisanii na ambacho mpaka sasa chashangaza wengi.

"Hii ni moja wapo msanii mkubwa East Africa. Msanii wa kike kutoka Pwani ambaye ndiye mkali zaidi ya wote East Africa. Msanii mwenye uzoefu na taaluma kubwa katika sanaa.Twazungumzia Ndogo Ndogo ambaye kwa muda sasa tumekuwa tukifanya kazi nae. Ni msanii mzuri si "uongo" na pia twashukuru kama kikundi kupata fursa kama hiyo.Ametusaidia sana hiyo si uongo, ni jambo hata mafans wanajua lakini pia vile vile kama dancers tumemsaidia tu si kwa show bali mambo mengi tu. Mara kwa mara tumekuwa tukifanya shows hata mazoezi na yeye ili kuhakikisha show iwe kali zaidi. Lakini mazoezi haya nikuwa hayachoshi tu ila pia ni kujitolea kunakotaka uvumilivu na kuelewa kwingi."

"Tumefanya shows nyingi mno na Video pia, ambayo utapata fursa kuitazama. Kujitolea kunakotaka uvumilivu na kuelewa kwingi. Tumefanya shows nyingi na video pia ambayo utapata fursa ya kuitazama(Mapanya). Yote tisa kumi, wakati huu kama kikundi tunahisi hili jambo limetukera sana, kutuvunja moyo kwa kuwa kikundi bora pwani wengi, mafans pia wana matarajio mengi nasi, haswa vile tunafanya kazi na msanii wa kike mzuri Pwanu nzima."

"Tulikuwa tumepanga mambo mengi makubwa na mazuri kama Team Nyota, hii ikiwa kufanya Videos zote,Kuvaa poa na pia kufanya kazi kubwa East Africa mzima na kwengineo. Ila si hivyo maanake safari hii kama kikundi tunahisi kuwekwa chini na mama yetu Nyota ambaye kwa kweli tunajituma sana kwa kazi yake. Na kama tulivyopanga nikuwa akitoka "Denmark" tutafanya video mbili moja wapo ikiwa ni pamoja na Frasha. Video ambayo kwetu kama kikundi tulikuwa tumeingoja sana na kujitayarisha vilivyo, ila kutemwa dakika za mwisho. Kwa mafans wetu inakera sana na najua hiyo video ikitoka wengi itawakera mbona madancer wake hawapo. Ni video ya aina yake kwakua ina gharama zaidi ju ya laki moja, na pia usishangae Frasha mwenyewe anatumiwa nauli ya ndege."

"Wakati sisi kwa show ni Matatu ama bus video ambayo vifaa vyake vywakodishwa na Elfu hamsini, lipo gari la kukodi na hoteli limetengwa kwa Frasha ila sisi kutoka apa Voi tu twakosa. Jambo la kuudhi kabisa si kwamba ni lazima tudance kwa hiyo Video, lakini kama Team Nyota kukosekana ndani ya hiyo video inavunja moyo. Sisi kama kikundi tumejua watu wengine wanamfaidi mama yetu Nyota hata kushinda sisi. Afadhali mlipwe hela chache lakini watu wasave kwa Video na Air tickets,kwani Frasha ni nani sanaa???? *Sababu anadaiwa kututoa kwa iyo Video... Jamani kwa mafans wote naomba tusaidiane hili jambo pamoja."

"Ingekuwa wewe ungehisi vipi? Video uliyoingoja kwa muda mrefu, kufanya mazoezi na kutembea mpaka kwa mama kwenda mazoezi, na ni lazima uvuke mto wa Voi paka huko. So far alitoka Denmark na sisi kama kikundi uniforms zenyewe hamna. Hili ndo jambo ambalo limetupa msukumo mkubwa sana wa kisani. Kwani kama kikundi tunaangazia kufanya kazi na Bahati karibuni...."

Here are behind the scene photos from the video shoot;

We reached out to Nyota Ndogo, and this is what he had to say about the allegations;

Nimeshangaa sana na hio story ndio nimepigiwa simu saizi. Wamesema hivyo nilikua nao juzi na tulifanya show vizuri sana Mombasa, na kila show tunayofanya nawaita tunakaa chini, iwe ya pesa kidogo tunafanya na iwe ya pesa kubwa pia tunafanya.